Tuesday, February 18, 2014

kwa wabongo wenzangu

Katika pita pita zangu huku bondeni, nimegundua kitu kimoja, wabongo jamani wameloea huku.. mh mpaka najiskia aibu...ukitembea tu kidogo.. unakisikia kiswahili kileee cha nyumbani.. wengi wanakaa tu kwenye vigenge na kupiga story zisizo na maana.. najiuliza swali.. sasa kama familia kule nyumbani zinawategemea; ndugu na jamaa wanasema kwamba kijana wetu bwana yuko kule ng'ambo akitafuta maisha na atatusaidia... kijana mwenyewe ndiye huyu ninayemuona hapa ambae kweli hata kujishughulisha, hajishughulishi...inakuweje? yaani natamani ningewakalisha semina miwape somo moja hilo! mbaya zaidi ninaambiwa nisije nikathubutu kufikiri kwamba wabongo wote marafiki zangu.. ndiyo siku kila nlichokibeba kitatolewa mikononi mwangu na maisha yangu kuwa hatarini.. mh kweli Mungu atusaidie... mara nyingi tunaisema serikali yetu na kuilaumu lakini kwa hawa huku je? inabidi tubadilishe mawazo yetu.. tuache fikra duni na hasi tufanye kazi kwa bidii na kuacha uvivu na ulegevu. badiliko linaanza na wewe...

No comments:

Post a Comment